Mt. 14:7-9 Swahili Union Version (SUV)

7. Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lo lote atakaloliomba.

8. Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.

9. Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe;

Mt. 14