20. Mwanzi uliopondeka hatauvunja,Wala utambi utokao moshi hatauzima,Hata ailetapo hukumu ikashinda.
21. Na jina lake Mataifa watalitumainia.
22. Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.
23. Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi?