Mt. 12:20-23 Swahili Union Version (SUV)

20. Mwanzi uliopondeka hatauvunja,Wala utambi utokao moshi hatauzima,Hata ailetapo hukumu ikashinda.

21. Na jina lake Mataifa watalitumainia.

22. Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.

23. Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi?

Mt. 12