39. Akawaagiza wawaketishe wote, vikao vikao, penye majani mabichi.
40. Wakaketi safu safu, hapa mia hapa hamsini.
41. Akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akashukuru, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi wake wawaandikie; na wale samaki wawili akawagawia wote.