Mk. 6:16-19 Swahili Union Version (SUV)

16. Lakini Herode aliposikia, alisema, Yohana, niliyemkata kichwa, amefufuka.

17. Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;

18. kwa sababu Yohana alimwambia Herode, Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo.

19. Naye yule Herodia akawa akimvizia, akataka kumwua, asipate.

Mk. 6