Mk. 5:21-25 Swahili Union Version (SUV)

21. Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng’ambo katika kile chombo, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari.

22. Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake,

23. akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi.

24. Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa.

25. Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili,

Mk. 5