20. Mkutano wakakusanyika tena, hata wao wenyewe wasiweze hata kula mkate.
21. Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana walisema, Amerukwa na akili.
22. Nao waandishi walioshuka kutoka Yerusalemu wakasema, Ana Beelzebuli, na, Kwa mkuu wa pepo huwatoa pepo.
23. Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?