8. Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.
9. Ikawa siku zile, Yesu alikuja kutoka Nazareti ya Galilaya, akabatizwa na Yohana katika Yordani.
10. Mara alipopanda kutoka majini, akaona mbingu zinapasuka, na Roho, kama hua, akishuka juu yake;
11. na sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.
12. Mara Roho akamtoa aende nyikani.