Mk. 1:16-18 Swahili Union Version (SUV)

16. Naye alipokuwa akipita kando ya bahari ya Galilaya, akamwona Simoni na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.

17. Yesu akawaambia, Njoni mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.

18. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.

Mk. 1