16. Naye alipokuwa akipita kando ya bahari ya Galilaya, akamwona Simoni na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.
17. Yesu akawaambia, Njoni mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.
18. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.