5. Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau;Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu.
6. Usimwache, naye atakuhifadhi;Umpende, naye atakulinda.
7. Bora hekima, basi jipatie hekima;Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
8. Umtukuze, naye atakukuza;Atakupatia heshima, ukimkumbatia.
9. Atakupa neema kuwa kilemba kichwani;Na kukukirimia taji ya uzuri.
10. Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu;Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.