Mit. 4:17-21 Swahili Union Version (SUV)

17. Maana wao hula mkate wa uovu,Nao hunywa divai ya jeuri.

18. Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing’aayo,Ikizidi kung’aa hata mchana mkamilifu.

19. Njia ya waovu ni kama giza;Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho.

20. Mwanangu, sikiliza maneno yangu;Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu.

21. Zisiondoke machoni pako;Uzihifadhi ndani ya moyo wako.

Mit. 4