Mit. 4:14-17 Swahili Union Version (SUV)

14. Usiingie katika njia ya waovu,Wala usitembee katika njia ya wabaya.

15. Jiepushe nayo, usipite karibu nayo,Igeukie mbali, ukaende zako.

16. Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara;Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.

17. Maana wao hula mkate wa uovu,Nao hunywa divai ya jeuri.

Mit. 4