14. Usiingie katika njia ya waovu,Wala usitembee katika njia ya wabaya.
15. Jiepushe nayo, usipite karibu nayo,Igeukie mbali, ukaende zako.
16. Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara;Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu.
17. Maana wao hula mkate wa uovu,Nao hunywa divai ya jeuri.