19. Mwendo wa tai katika hewa;Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba;Mwendo wa merikebu katikati ya bahari;Na mwendo wa mtu pamoja na msichana.
20. Hivyo ndivyo mwendo wa mwanamke mzinifu;Hula, akapangusa kinywa chake,Akasema, Sikufanya uovu.
21. Kwa ajili ya mambo matatu nchi hutetemeka,Naam, kwa ajili ya manne haiwezi kuvumilia.