10. Usimchongee mtumwa kwa bwana wake;Asije akakulaani, ukaonekana una hatia.
11. Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao;Wala hawambariki mama yao.
12. Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe;Ambao hawakuoshwa uchafu wao.
13. Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini!Na kope zao zimeinuka sana.
14. Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga;Na vigego vyao ni kama visu.Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu.