Mit. 3:4-9 Swahili Union Version (SUV)

4. Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri,Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.

5. Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;

6. Katika njia zako zote mkiri yeye,Naye atayanyosha mapito yako.

7. Usiwe mwenye hekima machoni pako;Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.

8. Itakuwa afya mwilini pako,Na mafuta mifupani mwako.

9. Mheshimu BWANA kwa mali yako,Na kwa malimbuko ya mazao yako yote.

Mit. 3