4. Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri,Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.
5. Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote,Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6. Katika njia zako zote mkiri yeye,Naye atayanyosha mapito yako.
7. Usiwe mwenye hekima machoni pako;Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.
8. Itakuwa afya mwilini pako,Na mafuta mifupani mwako.
9. Mheshimu BWANA kwa mali yako,Na kwa malimbuko ya mazao yako yote.