Mit. 3:18-20 Swahili Union Version (SUV)

18. Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana;Ana heri kila mtu ashikamanaye naye.

19. Kwa hekima BWANA aliiweka misingi ya nchi;Kwa akili zake akazifanya mbingu imara;

20. Kwa maarifa yake vilindi viligawanyika;Na mawingu yadondoza umande.

Mit. 3