1. Mwanangu, usiisahau sheria yangu,Bali moyo wako uzishike amri zangu.
2. Maana zitakuongezea wingi wa siku.Na miaka ya uzima, na amani.
3. Rehema na kweli zisifarakane nawe;Zifunge shingoni mwako;Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4. Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri,Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.