Mit. 28:24-27 Swahili Union Version (SUV)

24. Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa;Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.

25. Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina;Bali amtumainiye BWANA atawandishwa.

26. Mwenye kujitumainia moyo wake ni mjinga;Bali yeye aendaye kwa busara ataokolewa.

27. Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu;Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.

Mit. 28