4. Ondoa takataka katika fedha,Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;
5. Mwondoe asiye haki mbele ya mfalme,Na kiti chake cha enzi kitathibitika katika haki.
6. Usijitukuze mbele ya uso wa mfalme;Wala usisimame mahali pa watu wakuu;
7. Kwa maana ni heri kuambiwa, Njoo huku mbele;Kuliko kuwekwa nyuma machoni pa mkuu.Yale uliyoyaona kwa macho,
8. Usitoke nje kwa haraka ili kuyashindania;Usije ukakosa kujua la kutenda hatimaye,Mwenzako atakapokuwa amekuaibisha.