Mit. 25:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Ondoa takataka katika fedha,Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;

5. Mwondoe asiye haki mbele ya mfalme,Na kiti chake cha enzi kitathibitika katika haki.

6. Usijitukuze mbele ya uso wa mfalme;Wala usisimame mahali pa watu wakuu;

7. Kwa maana ni heri kuambiwa, Njoo huku mbele;Kuliko kuwekwa nyuma machoni pa mkuu.Yale uliyoyaona kwa macho,

8. Usitoke nje kwa haraka ili kuyashindania;Usije ukakosa kujua la kutenda hatimaye,Mwenzako atakapokuwa amekuaibisha.

Mit. 25