19. Ili matumaini yako uyaweke kwa BWANA, leo nimekujulisha wewe haya, naam, wewe.
20. Je! Sikukuandikia mambo makuu juu ya mashauri na juu ya maarifa;
21. ili kukujulisha hakika ya maneno ya kweli, uwarudishie wakutumao maneno ya kweli?
22. Usimnyang’anye maskini, kwa kuwa ni maskini;Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni;