Mit. 21:26-29 Swahili Union Version (SUV)

26. Kuna atamaniye kwa choyo mchana kutwa;Bali mwenye haki hutoa wala hanyimi.

27. Sadaka ya wasio haki ni chukizo;Si zaidi sana ailetapo mwenye nia mbaya!

28. Shahidi wa uongo atapotea;Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.

29. Asiye haki huufanya uso wake kuwa mgumu;Bali mtu mnyofu huzifikiri njia zake.

Mit. 21