Mit. 20:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Usipende usingizi usije ukawa maskini;Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

14. Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.

15. Dhahabu iko, na marijani tele;Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.

16. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.

17. Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.

Mit. 20