15. Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;Na nafsi yake mvivu itaona njaa.
16. Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake;Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.
17. Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA;Naye atamlipa kwa tendo lake jema.
18. Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini;Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.