Mit. 19:15-18 Swahili Union Version (SUV)

15. Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;Na nafsi yake mvivu itaona njaa.

16. Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake;Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.

17. Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA;Naye atamlipa kwa tendo lake jema.

18. Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini;Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.

Mit. 19