Mit. 18:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Yeye ajibuye kabla hajasikia,Ni upumbavu na aibu kwake.

14. Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake;Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?

15. Moyo wa mwenye busara hupata maarifa;Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.

16. Zawadi ya mtu humpatia nafasi;Humleta mbele ya watu wakuu.

17. Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki;Lakini jirani yake huja na kumchunguza.

Mit. 18