Mit. 17:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Amdhihakiye maskini humsuta Muumba wake;Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu.

6. Wana wa wana ndio taji ya wazee,Na utukufu wa watoto ni baba zao.

7. Maneno mazuri hayapendezi kinywani mwa mpumbavu;Siuze midomo ya uongo kinywani mwa mkuu.

8. Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;Kila kigeukapo hufanikiwa.

9. Afunikaye kosa hutafuta kupendwa;Bali yeye akashifuye neno hutenga rafiki.

10. Lawama hupenya moyoni mwa mwenye ufahamu,Kuliko mapigo mia moyoni mwa mpumbavu.

Mit. 17