8. Afadhali mali kidogo pamoja na haki,Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
9. Moyo wa mtu huifikiri njia yake;Bali BWANA huziongoza hatua zake.
10. Kukata maneno huwa katika midomo ya mfalme;Kinywa chake hakitakosa katika hukumu.
11. Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya BWANA;Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.