Mit. 15:20-26 Swahili Union Version (SUV)

20. Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;Bali mpumbavu humdharau mamaye.

21. Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili;Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.

22. Pasipo mashauri makusudi hubatilika;Bali kwa wingi wa washauri huthibithika.

23. Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!

24. Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;Ili atoke katika kuzimu chini.

25. BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi;Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.

26. Mashauri mabaya ni chukizo kwa BWANA;Bali maneno yapendezayo ni safi.

Mit. 15