Mit. 14:24-27 Swahili Union Version (SUV)

24. Taji ya wenye hekima ni mali zao;Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.

25. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;Bali atoaye uongo hudanganya.

26. Kumcha BWANA ni tumaini imara;Watoto wake watakuwa na kimbilio.

27. Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima,Ili kuepukana na tanzi za mauti.

Mit. 14