22. Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi;Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.
23. Chakula kingi chapatikana kwa ukulima wa maskini;Bali viko viharibiwavyo kwa sababu ya dhuluma.
24. Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe;Bali yeye ampendaye humrudi mapema.