Mit. 12:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA;Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.

3. Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu;Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.

4. Mwanamke mwema ni taji ya mumewe;Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.

5. Mawazo ya mwenye haki ni adili;Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.

6. Maneno ya waovu huotea damu;Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.

Mit. 12