Mit. 12:17-20 Swahili Union Version (SUV)

17. Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki;Bali shahidi wa uongo hutamka hila.

18. Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga;Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.

19. Mdomo wa kweli utathibitishwa milele;Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.

20. Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu;Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.

Mit. 12