23. Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu;Tazama, nitawamwagia roho yangu,Na kuwajulisheni maneno yangu.
24. Kwa kuwa nimeita, nanyi mkakataa;Nimeunyosha mkono wangu, asiangalie mtu;
25. Bali mmebatilisha shauri langu,Wala hamkutaka maonyo yangu;
26. Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu,Nitadhihaki hofu yenu ifikapo;
27. Hofu yenu ifikapo kama tufani,Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli,Dhiki na taabu zitakapowafikia.