8. Ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu na haki kuondolewa kwa jeuri katika jimbo, usilistaajabie jambo hilo; kwa sababu,Aliye juu kuliko walio juu huangalia;Tena wako walio juu kupita hao.
9. Lakini, pamoja na hayo, manufaa ya nchi kwa kila njia ni mfalme anayejibidiisha kwa ajili ya shamba.
10. Apendaye fedha hatashiba fedha,Wala apendaye wingi hatashiba nyongeza.Hayo pia ni ubatili.
11. Mali yakiongezeka, hao walao nao waongezeka na mwenyewe hufaidiwa nini, ila kuyatazama kwa macho yake tu?