Mdo 15:16-22 Swahili Union Version (SUV)

16. Baada ya mambo haya nitarejea,Nami nitaijenga tena nyumba ya Daudi iliyoanguka.Nitajenga tena maanguko yake,Nami nitaisimamisha;

17. Ili wanadamu waliosalia wamtafute Bwana,Na mataifa yote ambao jina langu limetajwa kwao;

18. Asema Bwana, ajulishaye hayo tangu milele.

19. Kwa sababu hiyo mimi naamua hivi; Tusiwataabishe wale waliomgeukia Mungu katika Mataifa;

20. bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu.

21. Kwa maana tangu zamani za kale Musa anao watu wahubirio mambo yake; katika kila mji husomwa kila sabato katika masinagogi.

22. Basi ikawapendeza mitume na wazee na kanisa lote kuwachagua watu miongoni mwao na kuwapeleka Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba; nao ni hawa, Yuda aliyeitwa Barsaba, na Sila, waliokuwa watu wakuu katika ndugu. Wakaandika hivi na kupeleka kwa mikono yao,

Mdo 15