Lk. 6:46-48 Swahili Union Version (SUV)

46. Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo?

47. Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.

48. Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana, na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa imejengwa vizuri.

Lk. 6