Lk. 5:37-39 Swahili Union Version (SUV)

37. Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; na kama akitia, ile divai mpya itavipasua vile viriba, divai yenyewe itamwagika, na viriba vitaharibika.

38. Lakini divai mpya sharti kutiwa katika viriba vipya.

39. Wala hakuna anywaye divai ya kale akatamani divai mpya; kwa kuwa asema, Ile ya kale ndiyo iliyo njema.

Lk. 5