28. Wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo.
29. Wakaondoka wakamtoa nje ya mji, wakampeleka mpaka ukingo wa kilima ambacho mji wao umejengwa juu yake, wapate kumtupa chini;
30. lakini yeye alipita katikati yao, akaenda zake.
31. Akashuka mpaka Kapernaumu, mji wa Galilaya, akawa akiwafundisha siku ya sabato;
32. wakashangaa mno kwa mafundisho yake, kwa kuwa neno lake lilikuwa na uwezo.