43. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
44. Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,
45. jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.
46. Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.