Lk. 22:28-33 Swahili Union Version (SUV)

28. Nanyi ndinyi mliodumu pamoja nami katika majaribu yangu.

29. Nami nawawekea ninyi ufalme, kama vile Baba yangu alivyoniwekea mimi;

30. mpate kula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu; na kuketi katika viti vya enzi, huku mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

31. Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

32. lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.

33. Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani au hata kifoni.

Lk. 22