Lk. 2:14-18 Swahili Union Version (SUV)

14. Atukuzwe Mungu juu mbinguni,Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.

15. Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya, na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha Bwana.

16. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini.

17. Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.

18. Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.

Lk. 2