Lk. 18:18-24 Swahili Union Version (SUV)

18. Tena, mtu mkubwa mmoja alimwuliza, akisema, Mwalimu mwema, nifanye nini ili nipate kuurithi uzima wa milele?

19. Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu.

20. Wazijua amri; Usizini, Usiue, Usiibe, Usishuhudie uongo, Waheshimu baba yako na mama yako.

21. Akasema, Hayo yote nimeyashika tangu utoto wangu.

22. Yesu aliposikia hayo alimwambia, Umepungukiwa na neno moja bado; viuze ulivyo navyo vyote, ukawagawanyie maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha, njoo unifuate.

23. Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.

24. Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu!

Lk. 18