Lk. 1:49-54 Swahili Union Version (SUV)

49. Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu,Na jina lake ni takatifu.

50. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizaziKwa hao wanaomcha.

51. Amefanya nguvu kwa mkono wake;Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;

52. Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi;Na wanyonge amewakweza.

53. Wenye njaa amewashibisha mema,Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.

54. Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;Ili kukumbuka rehema zake;

Lk. 1