Law. 26:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Msifanye sanamu yo yote, wala msijisimamishie sanamu ya kuchonga, wala mnara, wala msiweke jiwe lo lote lililochorwa katika nchi yenu ili kulisujudia; kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

2. Zishikeni Sabato zangu, na kupastahi patakatifu pangu; mimi ndimi BWANA.

3. Kama mkienda katika amri zangu, na kuyashika maagizo yangu, na kuyafanya;

4. ndipo nitazinyesha mvua zenu kwa nyakati zake, na nchi itazaa maongeo yake, na miti ya mashambani itazaa matunda yake.

5. Tena kupura nafaka kwenu kutaendelea hata wakati wa kuvuna zabibu, na kuvuna zabibu kutaendelea hata wakati wa kupanda mbegu; nanyi mtakula chakula chenu na kushiba, na kuketi katika nchi yenu salama.

Law. 26