Law. 24:15-19 Swahili Union Version (SUV)

15. Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake atachukua dhambi yake.

16. Na yeye atakayelikufuru jina la BWANA hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzalia, hapo atakapolikufuru jina la BWANA atauawa.

17. Na mtu ampigaye mtu hata akafa, lazima atauawa;

18. na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.

19. Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;

Law. 24