Kut. 33:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Basi, sasa nakuomba, ikiwa nimepata neema mbele zako, unionyeshe njia zako, nipate kukujua, ili nipate neema mbele zako; ukakumbuke ya kuwa taifa hilo ndilo watu wako.

14. Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.

15. Naye akamwambia, Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue kutoka hapa.

16. Kwa maana itajulikanaje kuwa nimepata neema mbele zako, mimi na watu wako? Siyo kwa sababu unakwenda pamoja nasi, hata mimi na watu wako tutengwe na watu wote walio juu ya uso wa nchi?

Kut. 33