Kut. 30:18-22 Swahili Union Version (SUV)

18. Fanya na birika la shaba, na tako lake la shaba, ili kuogea; nawe utaliweka kati ya hema ya kukutania na madhabahu, nawe utalitia maji.

19. Na Haruni na wanawe wataosha mikono yao na miguu yao humo;

20. hapo waingiapo ndani ya hema ya kukutania; watajiosha majini, ili wasife; au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike, kumteketezea BWANA sadaka ya moto;

21. basi wataosha mikono yao na miguu yao ili kwamba wasife; na neno hili litakuwa amri kwao milele, kwake yeye na kwa wazao wake katika vizazi vyao vyote.

22. Kisha BWANA akasema na Musa, na kumwambia,

Kut. 30