Kut. 15:19-21 Swahili Union Version (SUV)

19. Kwa maana farasi za Farao na magari yake na wapanda farasi wake waliingia ndani ya bahari, BWANA akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari.

20. Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.

21. Miriamu akawaitikia,Mwimbieni BWANA kwa maana ametukuka sana;Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.

Kut. 15