11. Ee BWANA, katika miungu ni nani aliye kama wewe?Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu,Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu?
12. Ulinyosha mkono wako wa kuume,Nchi ikawameza.
13. Wewe kwa rehema zako umewaongoza watu uliowakomboa,Kwa uweza wako uliwaelekeza hata makao yako matakatifu.
14. Kabila za watu wamesikia, wanatetemeka,Wakaao Ufilisti utungu umewashika.
15. Ndipo majumbe wa Edomu wakashangaa,Watu wa Moabu wenye nguvu tetemeko limewapata,Watu wote wakaao Kanaani wameyeyuka.
16. Hofu na woga umewaangukia;Kwa uweza wa mkono wako wanakaa kimya kama jiwe;Hata watakapovuka watu wako, Ee BWANA,Hata watakapovuka watu wako uliowanunua.