Kum. 28:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako.

3. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

4. Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.

5. Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.

6. Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.

Kum. 28