Kum. 22:8-11 Swahili Union Version (SUV)

8. Utakapojenga nyumba mpya, fanya ukuta kando-kando ya dari lako, usije ukaleta damu juu ya nyumba yako, mtu akianguka huko.

9. Usipande shamba lako la mizabibu aina mbili za mbegu; yasije yakaondolewa matunda yote, mbegu ulizopanda na maongeo ya mizabibu yako.

10. Usilime kwa ng’ombe na punda wakikokota jembe pamoja.

11. Usivae nguo iliyochanganyikana sufu na kitani pamoja.

Kum. 22