Kum. 19:18-21 Swahili Union Version (SUV)

18. nao waamuzi na watafute kwa bidii; na tazama, yule shahidi akiwa shahidi wa uongo, naye ametoa ushahidi wa uongo juu ya nduguye;

19. ndipo mtamfanyia kama alivyodhani kumfanyia nduguye; ndivyo utakavyoondoa uovu katikati yako.

20. Na watakaosalia watasikia na kuogopa, wasifanye tena uovu mfano wa huo katikati yako.

21. Wala jicho lako lisiwe na huruma; uzima kwa uzima, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.

Kum. 19